ASKARI ALIYEMUUA MWANGOSI AFUNGWA MIAKA 15 JELA.


Image result for PACIFIUS SIMON





Askari wa kikosi cha  kutuliza ghasia (FFU) mwenye  namba G .2573 Pacificius Cleophace Simon (27)  

MAHAKAMA  kuu ya Tanzania  kanda  ya  Iringa  leo  imemuhukumu kwenda  jela miaka  15 kwa kosa la mauaji  ya  bila  kukusudia  askari wa kikosi cha  kutuliza ghasia (FFU) mwenye  namba G .2573 Pacificius Cleophace Simon (27)  aliyemuua mwandishi  wa  habari  wa  kituo  cha Chanel Ten Daudi  Mwangosi.

Maamuzi hayo yametolewa leo baada ya kesi hiyo kuahirishwa juzi na Jaji Paul kihwelo ambaye alipitia utetezi wa mshitakiwa na maoni ya Wazee wa Baraza,ambapo mshtakiwa huyo alitiwa hatiani kwa kosa la kuua bila kukusudia na hukumu yake ingetolewa leo.












No comments

Powered by Blogger.