WANASAYANSI WATABILI KUPATWA KWA JUA KIPETE



Wanasayansi kutoka chuo kikuu huria Tanzania wamethibitisha kuwapo kwa tukio la kupatwa kwa jua kipete mwezi septemba kwenye usawa wa nchi yetu hasa maeneo ya kusini na jirani.
Mtaalam wa Astronomia na Mhadhiri wa fizikia kitivo cha sayansi,Teknolojia na Elimu ya Mazingira Chuo kikuu huria Dr. Noorali jiwaji ameeleza tukio hilo kuwa ni la kihistoria na hutokea kwa nadla sana maana jua huonekana kama pete badala ya mviringo.

Dr.Noorali kushoto akionyesha sampuli ya chujio maalumu ya mwanga na pembeni yake ni makamu mkuu wa chuo kikuu huria Tanzania Prof.Elifas Bisanda.

Dr Noorali amesema , tarehe 1 septemba ,kuanzia saa 4 asubuhi hadi 8 alasiri ,wakazi wa Rujewa kusini mwa Tanzania, karibu na Mbeya watashuhudia duara la jua linavyobadilika kuwa pete ya jua huku watanzania kote nchini wataona jua kali la utosini likimegwa kwa Zaidi ya 90% kwa kufunikwa na mwezi na kuliacha jua lionekane kama hilali nyembamba au kama mwezi mwandamo.
“Tarehe 1 septemba,Watanzania wanaoishi mikoa ya kusini wataona jua kama pete kwa dakika chache, wakati Tanzania kote pamoja na wa kusini wataona jua limepatwa kihilali kwa masaa manne”alisema.



Aidha, ametaja maeneo mengine ya kusini ambayo jua litapatwa kipete kuwa ni Katavi,Rukwa,Mbeya,Njombe,Ruvuma na Mtwara na sehemu zote za Afrika na Madagaska,huku akiwataka watu kutumia chujio maalum ya mwanga ili kuepuka madhara ya mionzi  ya jua kama wataangalia moja kwa moja au kutumia vifaa vingine vya kiza vilivyotengenezwa kienyeji, huku akisifu jitihada za kampuni ya SBC kwa kuahidi kudhamini vichujio 50,000 vya mwanga vitavyosambazwa mashuleni.
Hii si mara ya kwanza kutokea kwa tukio hili nchini kwani julai 31, 1962, miaka 54 iliyopita ,  April 18, 1977 miaka 33 iliyopita na likipita litatokea tena mei 21, 2031 miaka 15 ijayo na feb 17, 2064 baada ya miaka 48, hivyo ni tukio la kihistoria na la kujifunza kwa wanafunzi wanaopenda masomo ya sayansi.


No comments

Powered by Blogger.