ASKARI POLISI WAUWAWA DAR,NCHEMBA AWATAKA WALIOHUSIKA KUJISALIMISHA.

TUNAOMBA RADHI KWA BAADHI YA PICHA UTAKAZOZIONA.

ASKARI polisi 4 wameuawa kwa kupigwa risasi na majambazi huko Mbagala, mbande jijini Dar es Salaam usiku wa kuamkia leo.


Inadaiwa kuwa askari hao walikuwa wakibadilishana lindo katika Benki ya CRDB, tawi la Mbagala mbande na mara wakaibuka watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi na kuanza kuwashambulia kwa risasi na baada ya shambulizi hilo wanadaiwa kuondoka na pikipiki wakielekea maeneo ya Mvuti.


Polisi waliouawa ni pamoja na;

E5761 CPL YAHAYA

F4660 CPL HATIBU

G9544 PC TTITO.


Inasemekana kuwa tukio hilo limetokea mnamo saa 1: 30 usiku katika na inadaiwa kuwa wahalifu hao waliondoka na silaha moja aina ya SMG.


Mmoja kati ya polisi waliouawa alikuwa anaingia lindo, mmoja alikuwa anatoka na mwingine alikuwa dereva na imeelezwa kuwa majambazi hayo hayakuingia ndani ya benki ila gari la polisi (Leyland Ashok) limeharibiwa  kwa risasi.


Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro amethibitisha kutokea kwa tukio hilo: “Ni kweli kumetokea tukio la uvamizi hapa Mbagala lakini taarifa kamili nitazitoa kesho kwa kuwa bado nipo eneo la tukio kwa ajili ya uchunguzi zaidi”. Alisema Kamanda Sirro.

 "Usiku huu nimefika Mbande-Temeke,eneo lilipofanyika tukio baya la uhalifu wa kutumia silaha ambapo watu/majambazi zaidi ya saba wakiwa na silaha wamevamia eneo la Benki ya CRDB-Mbande na kuua askari  4 waliokuwa wakishuka  kwenye gari tayari kwa kupokezana lindo.





Pia wamejeruhi raia wa kawaida wawili,nimewajulia hali zao na wote wanaendelea vizuri.




Hatutaishia kulaani tu tukio hili na matukio mengine kama haya,natoa rai kwa wahusika kujisalimisha.Vilevile wananchi na raia wema tunaomba ushirikiano wenu katika vita hii ya kupambana na wahalifu hawa na wanaotuzunguka kwenye maeneo yetu."



Mwigulu Nchemba


23.08.2016



No comments

Powered by Blogger.